WELCOME

Thursday, July 11, 2013

ENJOY THE GREATEST QUOTES FROM MWINYI ALLY ABUU

Mwinyi Ally Abuu
"Hakika kile kilicho kigumu kwako ni chepesi kwa mwenzio, hivyo hivyo na kile kilicho kigumu kwa mwenzio ni chepesi kwako." Mwinyi Ally Abuu.

"Kila jambo huwa na makusudio yake, hauwezi ishi bila kukumbana na mitihani katika ulimwengu huu. Maana tuliumbwa kwa majaribio hivyo hatuna budi kukabiliana nayo." Mwinyi Ally Abuu

"Kila jambo huwa na makusudio yake, hauwezi ishi bila kukumbana na mitihani katika ulimwengu huu. Maana tuliumbwa kwa majaribio hivyo hatuna budi kukabiliana nayo." Mwinyi Ally Abuu

"Nothing will be easy until you work hard on it. So tied this life, I'm still on the truck yet on the destination. God show me the way I can go." Mwinyi Ally Abuu

"I used to have a girlfriend in previous days ambaye nilikuwa nampa pesa kila anapokohoa, alinipenda sana nami nikajiona napendwa. Lakini pesa ni maua kuna wakati uchanua na wakati usinyaa, sasa kuna kipindi mambo yangu yakawa siyo safi, yale mapenzi moto moto niliyokuwa nayapata kwa kimwana yule nayo yakapotea. Mwisho wa siku akaniona mimi wa kazi gani maana hapati pesa tena kama ilivyo mwanzo ndipo alipoamua kuachana na mimi na kuondoka na moyo wangu ambao nilimkabidhi takribani miaka tisa. So when a woman love you, inatakiwa ujiulize mara mbilimbili kama kweli upendo huo unatoka moyoni au kinywani mwake. Maana miongoni mwa wanawake wengi waigizaji hawakosekani." Mwinyi Ally Abuu

"In human life one person's gain is another person's loss." Mwinyi Ally Abuu

"Laiti tungeyajua ya kesho tungeyafanya ya leo kuwa mazuri, nawatakia jioni njema watu wangu." Mwinyi Ally Abuu

"Maisha haya ukifa unaweza kuwa maarufu zaidi ya uhai wako." Mwinyi Ally Abuu

"Ukimnya wa rafiki yako unauma kuliko kelele za adui yako, habari zenu waungwana? Kama mpo poa nawatakia siku njema." Mwinyi Ally Abuu

"Bora ya jana uliyoiona kuliko ya kesho usiyoitambua. Usiku mwema waungwana." Mwinyi Ally Abuu

"Wasiokubali ya wengi wanayakwao moyoni." Mwinyi Ally Abuu

"Roho mbaya siyo mtaji useme utakusaidia maishani, kuishi na watu vizuri ndiyo mpango mzima." Mwinyi Ally Abuu

"Daima ulichonacho mkononi ndicho chenye thamani zaidi" Mwinyi Ally Abuu

 "Elimu bila busara ni sawa na kutosoma," Mwinyi Ally Abuu

"Usipende shadadia kuwa kesho utafanya hiki na kile, hali ya kuwa ujui sekunde yako ya mwisho ni ipi katika dunia hii. Sasa ni bola zaidi ya kesho, nawatakia mchana mwema waungwana." Mwinyi Ally Abuu

"Si kila akuchekeae ni mwema kwako, binadamu ni viumbe wa ajabu sana." Mwinyi Ally Abuu

"Amini nawaambia mbegu isipokufa itabaki kuwa kama ilivyo ila ikifa itatoa matunda mema. Nawatakia usiku mwema." Mwinyi Ally Abuu

"Ukitaka kujua uzuri na ubaya wa mtu mfanye akasilike, maana atakuonesha yale yaliyofichika juu yake. Na penye mafanikio siku zote pana husuda ndani yake, lakini tambua walimwengu si wenye vitimbi zaidi ya Mwenyezi Mungu, maana yeye ndio mjanja na muelevu wa yote." Mwinyi Ally Abuu

"Hakuna kazi ngumu kama kusoma, yani nywele zitaninyonyoka mpaka basi maana elimu ya kibongo si mchezo" Mwinyi Ally Abuu

"Hakika mauti yanatosha kuwa mawaidha, jiite jina zuri upendalo mwisho wa siku utaitwa marehemu. Ishi katika nyumba nzuri upendayo, nyumba yako ya mwisho ni kaburi. Panda vyombo vizuri na vya kifahari mwishoe utapakiwa kwenye jeneza. Safiri katika dunia hii kwenda utakako lakini tambua safari yako ya mwisho ni umauti. Kama unaakili basi utaishi na watu vizuri, nawatakia mchana mwema na Mungu awabariki nyote." Mwinyi Ally Abuu

"Yafurahie matatizo yako ya sasa kwani ndio mafanikio yako ya baadae. Uwatafutao leo kesho watakutafuta na wakuchukiao sasa muda ukifika watakupenda maana kila chenye mwanzo huwa na mwisho, pia wakupao moyo sasa usiwasahau maana ndio chanzo cha mafanikio yako. Nawatakia usiku mwema na mafanikio katika maisha yenu." Mwinyi Ally Abuu

"Shukuru kwa kile kidogo ulichonacho maana kuna watu hata icho kidogo ulichonacho hawana. Alafu usishangae kuona watu wenye roho mbaya maana walikuwepo toka enzi na enzi. Watu wanaoiga akili za shetani kumnyang'anya madaraka Mungu na kuuona ulimwengu huu ni wakwao na kusahau kuwa kila uma utauonja umauti" Mwinyi Ally Abuu

"Ukitaka kuishi na watu vizuri jishushe na kila mtu umuone kama yupo juu yako, kuwa kwako Mercedes Benz usiwadharau Toyota Corolla. Maana hautajua nani anamsaada katika maisha yako. Nawatakia mchana mwema." Mwinyi Ally Abuu

"Japo imeandikwa samehe saba mara sabini, eeee Mungu muumba wa mbingu na ardhi na vitu vyote vilivyomo katika ulimwengu, kwa hawa wanaojiita miungu watu wanaowafanyia mabaya wenzao usiku na mchana, mi siwezi wasamehe kamwe. Najua hawana uwezo zaidi yako muumba wangu nami napiga goti kwako kwa uwezo wako Yalabi mikosi na mabaya yote iwafiki wenyewe." Mwinyi Ally Abuu

"Usiwachukie watu kwa sura zao, wapende kwa tabia zao, usiwaamini watu kwa kauli zao, washuhudie kwa matendo yao, usiwadharau watu kwa ufukara wao, waheshimu kwa utu wao, usiwajali watu kwa kipato chao, wape heshima kwa imani zao, usiwabeze watu kwa udini wao bali wahurumie kwa udhaifu wao. Mungu atuwezeshe haya, nawapenda nyote." Mwinyi Ally Abuu

"Ukipewa salamu na mtu ambae ni tofauti na jinsia yako haimaanishi amekupenda. Sisi ni binadamu kujuliana hali ni jambo jema, kama salamu ni kupenda basi nimependa wengi. Jamani mambo vp?" Mwinyi Ally Abuu

"Friends can be more dangerous than enemies." Mwinyi Ally Abuu

"Uzuri wa m2 upo kwa aliependa, kwa hiyo usishangae kuona mtu fulani kumpenda mtu fulani." Mwinyi Ally Abuu

"UKIPENDA Hakuna anaeamini kama unapenda, UKIUMIA Hakuna anaehisi maumivu yako, UKILIA Hakuna anaethamini kilio chako, ILA UKIJAMBA kila mtu JICHO KWAKO." Mwinyi Ally Abuu

"Uamuzi wowote ni bola kuliko kutokuwa na maamuzi" Mwinyi Ally Abuu